Matthew 5:1-6

(Mathayo 5–7)

Sifa Za Aliyebarikiwa

(Luka 6:20-23)

1 aBasi Isa alipoona makutano, alipanda mlimani akaketi chini, nao wanafunzi wake wakamjia. 2Ndipo akaanza kuwafundisha, akisema:
3 b“Heri walio maskini wa roho,
maana Ufalme wa Mbinguni ni wao.

4 cHeri wale wanaohuzunika,
maana hao watafarijiwa.

5 dHeri walio wapole,
maana hao watairithi nchi.

6 eHeri wenye njaa na kiu ya haki,
maana hao watatoshelezwa.
Copyright information for SwhKC